Submit your work, meet writers and drop the ads. Become a member
Jun 2014
NAKUSHUKURU
Baba nakushukuru kwa kunipa uhai hata sasa,
Nashukuru kwa kunisamehe na kunitakasa,
Nashukuru kwa kuwa ulikufa kwa ajili yangu,
Nashukuru kwani ulinibariki toka tumboni mwa mama yangu,
Nashukuru unanipenda hata na mapungufu yangu,
Nashukuru kwa kuwa unanilinda kutoka na kuingia kwangu,
Lihimidiwe jina lako YEHOVA hakuna kama wewe,
Mungu kwa kuwa hakuna kinachoweza kulinganishwa na upendo wako,
Hakuna kinachoweza kulinganishwa na wema wako,
Je ni mwanadamu gani awezaye kufa kwa ajili ya asimjua?
Ni nani awezaye kukubali kuteseka kwa niaba ya yule amchukiaye?
Ni nani awezaye kuuweka chini uhai wake kwa ajili ya adui yake?
ISSAI MASHINGO
Written by
ISSAI MASHINGO  ARUSHA- TANZANIA
(ARUSHA- TANZANIA)   
1.5k
 
Please log in to view and add comments on poems