Hello Poetry
Submit your work and get some sparkles! Create free account
"mungu" poems
Hapa ndipo umenifikisha Umalenga na ujopo Wa kiingereza tulimudu lakini kiswahili kitamu **** la mama litamu Hata liwe la mbwa Kimombo kilaini majineno Kama mayai ya johari Kuangaza mitima halaiki Namshukuru Rabuka Kwa talanta ya kuandika Tukaumba kwa maneno Waumbaji nikawaunga Kama yeye Mungu, Nguvu za maneno kat'tunukia Uwezo wa karana hii Kuwateka akilizo Nyika na mito kuwavusha Hadi sayari za ndoto zao Uswahilini narudi mie Kitamu kwelikweli Nashukuru Maulana Kipaji nilipata Naye ataniauni Dau langu lifike kilindini Nitue kileleni Niangaze kama Zuhura Hapa ndipo nimefika Umalenga na ujopo N'taukumbatia milele Kwa Kiswahili na kimombo Mitima zao kusisimua.
0
Jan 6, 2016
Jan 6, 2016 at 8:03 AM UTC
Kiswahili Kirembo
NAKUSHUKURU Baba nakushukuru kwa kunipa uhai hata sasa, Nashukuru kwa kunisamehe na kunitakasa, Nashukuru kwa kuwa ulikufa kwa ajili yangu, Nashukuru kwani ulinibariki toka tumboni mwa mama yangu, Nashukuru unanipenda hata na mapungufu yangu, Nashukuru kwa kuwa unanilinda kutoka na kuingia kwangu, Lihimidiwe jina lako YEHOVA hakuna kama wewe, Mungu kwa kuwa hakuna kinachoweza kulinganishwa na upendo wako, Hakuna kinachoweza kulinganishwa na wema wako, Je ni mwanadamu gani awezaye kufa kwa ajili ya asimjua? Ni nani awezaye kukubali kuteseka kwa niaba ya yule amchukiaye? Ni nani awezaye kuuweka chini uhai wake kwa ajili ya adui yake?
0
Jun 26, 2014
Jun 26, 2014 at 6:07 AM UTC
NAKUSHUKURU